Masharti na Vigezo

Karibu Almasi – Afrimarketstore

Unapotumia soko letu la kidijitali kununua au kuuza bidhaa, unakubaliana na masharti yafuatayo ya matumizi. Tafadhali yasome kwa makini.

1. Usajili wa Akaunti

  1. Wauzaji na Wateja: Kila mtumiaji lazima atoe taarifa za kweli na namba ya simu inayofanya kazi wakati wa usajili.
  2. Ulinzi: Ni wajibu wako kulinda nenosiri (password) la akaunti yako. Almasi haitahusika na hasara yoyote itakayotokana na uzembe wako.

2. Masharti ya Uuzaji na Malipo

  1. Malipo ya Kabla (Pre-paid): Ili kulinda mitaji ya wauzaji, wateja wote wanatakiwa kukamilisha malipo kwa njia salama za kidijitali zilizopo kwenye mfumo kabla ya mzigo kusafirishwa.
  2. Kamisheni ya Soko: Almasi itakata asilimia (8%) ya makubaliano kwa kila mauzo yaliyofanyika kupitia jukwaa hili.
  3. Marufuku: Ni marufuku kwa muuzaji na mteja kufanya biashara au malipo nje ya mfumo wa Almasi kwa kutumia taarifa zilizopatikana hapa.

3. Usafirishaji na Mizigo

  1. Uwasilishaji: Wauzaji wana wajibu wa kufunga na kuwasilisha mzigo kwenye kampuni ya usafirishaji ndani ya muda uliopangwa baada ya kupokea oda.
  2. Ufuatiliaji: Mteja atapewa namba ya ufuatiliaji wa mzigo wake hadi utakapomfikia mkoani kwake.

4. Sheria Inayotumika

  • Masharti haya yanatawaliwa na kulindwa chini ya sheria za Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

0
Scroll to Top